Vidonge vya iodini

 Baraza la Kijiji ya Tønsberg wako na vidonge vya iodini vya kutosheka wenye watapendekezwa.

Vijiji zote mu norwe waliombwa kuwa na vidonge vya kutosheka wakaaji, kwa sababu ya vita yenye inapitika mu Ukraine. Kama mutu anapata sumu ya mnururisho/mionzi mu mwili, kutumia kidonge ya iodini itapunguza usikuwe mu hatari ya kupata kansere ya dundumio.Vidonge vya iodini vinapaswa kukamatiwa mara imoja tu, wakati mfiduo wa iodini ya mionzi ni mingi zaidi.

Shirika ya Kulinda Mionzi na Maandalizi ya Nyuklia (DSA) ahitazamie kama mionzi  ya bombe itafika Norwe kutoka Ukraina na kama wakaaji watahitaji kukamata vidonge vya iodini.

Mamlaka za afya za kitaifa wataamua ni wakati gani ndio watatoa pedekezo ya kukumata kidonge ya iodini.

Nani anapaswa ku kamata vidonge vya iodini?

Wenye wanapaswa kutumia iodine ni watoto na vijana wa mwaka chini ya kumi na munane(18), wanawake wenye wako mimba ao wenye kunyonyesha, kama wanapata mionzi mu mwili kutoka ku bombe ya nyuklia. Kama hali inakuwa mubaya sana serikali(mamlaka ya kitaifa) itapendekeza wale wenye wako na mwaka chini ya makumi ine (40) kukamata nao pia kidonge ya iodini. Serikali(mamlaka ya kitaifa) itatowa ratiba wakati uyo.

Nani apaswe tumia vidongo vya iodini?

Mutu yeyote mwenye iko na mwaka zaidi ya makumi ine(40).  Ukisha pitisha mwaka makumi ine(40 ) hauko mu hatari ya kupata kansere, pia iodini inaweza kuongeza hatari ya ugonjwa mu dundumio  na mazara yanayohusiana na iodini.

Ikiwa uko na ugonjwa fulani ao unatumia vidonge venye hauwezi changa na iodini, usitumie iodini. Ikiwa hauna uhakika kama kuna sababu za matibabu zenye kukuzuia wewe usitumiye iodini, lazima ufafanue iyo na  munganga wako.

Watu wenye walipasuliwa ku dundumio awahitaji kutumia iodini.

Masomo, chekechea na vituo vya afya

Vidonge vya Iodini vitachungwa kumasomo, masomo za chekechea na ku vituo vya afya. Ikihitajika vidonge vitatolewa haraka kwa wana inchi. Kama kunatokea hali kwenye vidonge vinapaswa kuchukuliwa wakati watoto wako kumasomo, masomo na chekechea zitakuwa na jukumu la kupatia watoto vidonge. Ili masomo ipate fursa ya kufanya vile, ni lazima wazazi ao walezi wa patie masomo ruhusa.

Wenye wako mimba, wenye kunyonyesha na watoto wadogo sana watapata vidonge ya iodini ku vituo vya afya. Watu wenye wako na ujuzi wa afya wataweza kutoa mwongozo kuhusu kipimo sahihi, na ikiwezekana kusaidia kuwapa watoto wadogo sana vidonge